MPRU KUZINDUA BOTI MPYA YA KISASA HIVI KARIBUNI
MPRU KUZINDUA BOTI MPYA YA KISASA HIVI KARIBUNI

Tarehe Iliyochapishwa: Alhamisi, Novemba 09, 2023

Baadhi ya wajumbe wa Menejimenti ya Hifadhi za Bahari na Maeneo Tengefu (MPRU) leo tarehe 09 Novemba, 2023 jijini Dar Es Salaam yatembelea na kukagua utengenezwaji wa Boti ya Kisasa ya kitalii aina ya Glass Bottom Boat katika yadi ya  Songoro Marine, iliyopewa jina la MV Dodoji II inayotarajiwa kuzinduliwa hivi karibuni.

Aidha, boti hii inatarajiwa kuchochea ukuaji wa sekta ya utalii katika vivutio vya maeneo ya bahari  Tanzania, kwa wageni kutondoka ndani na nje ya nchi.